WIZARA YA ELIMU KUENDELEA KUTENGA BAJETI YA KUNUNUA VIFAA VISAIDIZI KWA WANAFUNZI WALEMAVU.


Waziri wa elimu sayansi tekinolojia na mafunzo ya ufundi Mh Joyce Ndalichako amesema kuwa wizara yake itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya kununua vifaa visaidizi kwa wanafunzi wenye ulemavu.

Image result for PICHA YA JOYCE NDALICHAKO
MH. NDALICHAKO
Mh Ndalichako ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu maswali ya wabunge bungeni ambapo amesema kuwa serikali inafahamu changamoto mbalimali zinazowakabili wanafunzi wenye ulemavu ikiwemo miundombinu ya majengo na vifaa vya kujifunzia hivyo kwa mwaka huu imetenga bajeti kwa ajili ya kupunguza changamoto hizo.

Kwa upande wake naibu waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu anayeshughulikia walemavu Mh Stella Ikupa amesema kuwa ili kupunguza gharama za vifaa kwa walemavu ikiwemo miguu bandia serikali imefuta kodi kwa vifaa hivyo ambavyo vinaagizwa kutoka nje ya nchi. 

Aidha amesema kuwa lengo la serikali kuondoa kodi hizo ni ili walemavu wanaohitaji vifaa hivyo wavipate kwa gharama nafuu.

Hata hivyo bunge la bajeti linaendelea mkoani Dodoma ambapo wabunge wanaendelea kujadili bajeti za wizara mbalimbali kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019.

WIZARA YA ELIMU KUENDELEA KUTENGA BAJETI YA KUNUNUA VIFAA VISAIDIZI KWA WANAFUNZI WALEMAVU. WIZARA YA ELIMU KUENDELEA KUTENGA BAJETI YA KUNUNUA VIFAA VISAIDIZI KWA WANAFUNZI WALEMAVU. Reviewed by safina radio on April 11, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.