SERIKALI YASEMA HAKUNA FEDHA YEYOTE ILIYOPOTEA


Serikali kupitia wizara ya fedha na mipango imesema kuwa hakuna fedha yoyote ya serikali ya shilingi trilioni 1.51iliyopotea au kutumika kwa matumizi ambayo hayakuidhinishwa na bunge.

Image result for PICHA YA ASHANTU KIJAJI NAIBU WAZIRI WA FEDHA
NAIBU WAZIRI WA FEDHA ASHANTU KIJAJI
Kauli hiyo imetolewa na naibu waziri wa fedha na mipango Mh Ashantu Kijaji bungeni mjini Dodoma wakati akitoa kauli ya serikali bungeni kuhusiana na taarifa zinazoenezwa na baadhi ya watu kuwa kiasi cha shilingi trilioni 1.51 ambazo ni fedha za serikali hazijulikani zilipo.

Mh Kijaji amesema kuwa kwa kipindi cha mwaka wa 2012/2017 serikali kupitia wizara ya fedha na mipango ilikuwa kwenye kipindi cha mpito cha miaka mitano ya utekelezaji wa mpango mkakati wa kuandaa hesabu za serikali kwa mfumo wa viwango vya kimataifa vya uhasibu katika sekta ya umma hivyo kutokana na taarifa za mfumo huo inaonesha kuwa hakuna fedha yoyote ya serikali iliyopotea.

Ameongeza kuwa kutokana na ufafanuzi huo taarifa zinazoenezwa na baadhi ya watu kuwa kiasi hicho cha fedha matumizi yake hayajulikani hayana msingi wala mantiki yoyote na hawaitakii mema serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dr John Magufuli.

Hata hivyo Mh Kijaji amewataka wabunge na wananchi kutambua kuwa serikali ya awamu ya tano ipo makini na haiwezi kuruhusu kwa namna yoyote ile upotevu wa fedha za umma na dhamira ya serikali ni kuhakikisha kuwa mapato yanayokusanywa hapa nchini yanatumika kwa maslahi ya wananchi wote.


SERIKALI YASEMA HAKUNA FEDHA YEYOTE ILIYOPOTEA SERIKALI YASEMA HAKUNA FEDHA YEYOTE ILIYOPOTEA Reviewed by safina radio on April 20, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.