SERIKALI KUENDELEA KUTOA ELIMU KUHUSU ATHARI ZA KIFUA KIKUU


Serikali imesema kuwa inaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu athari za ugonjwa hatari wa kifua kikuu (TB) Kwa kupitia vyombo mbalimbali vya habari pamoja na mitandao ya kijamii.

Image result for PICHA YA FAUSTINE NDUGULILE NAIBU WAZIRI WA AFYA
NAIBU WAZIRI WA AFYA FAUSTINE NDUGULILE
Hayo yemeelezwa leo bungeni mjini Dodoma na naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh Faustine Ndugulile wakati akijibu swali la mbunge wa Mtambile Mh Masood Abdalah aliyetaka kujua serikali imejiwekea mikakati gani ya kupambana na ugonjwa wa kifua kikuu hapa nchini.

Amesema kuwa lengo la serikali la kutoa elimu hiyo ni ili wananchi wajue madhara ya ugonjwa huo ili waweze kuwahi katika vituo vya afya mapema kwa kuwa matibabu ya kifua kikuu hutolewa bure.

Aidha naibu waziri Ndugulile amefafanua kuwa ugonjwa wa kifua kikuu huwapata hasa watoto wadogo wenye umri chini ya miaka mitano,wazee,wafungwa na watu wenye virusi vya ukimwi,ambapo pia hushambulia maeneo mbalimbali ya mwili ikiwemo mapafu,moyo,ngozi na kila kiungo cha mwili.

Mh waziri pia amewataka wabunge kushirikiana na serikali katika kutoa elimu kwa wananchi katika maeneo yao wanayoishi ili wajue namna ya kukabiliana na ugonjwa huo unaoambukizwa kwa njia ya hewa na kuwahi matibabu mapema kwani ugonjwa wa kifua kikuu unatibika.

Hata hivyo bunge la bajeti linaendelea bungeni mjini Dodoma ambapo leo waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano Mh Makame Mbarawa amewasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019.



SERIKALI KUENDELEA KUTOA ELIMU KUHUSU ATHARI ZA KIFUA KIKUU SERIKALI KUENDELEA KUTOA ELIMU KUHUSU ATHARI ZA KIFUA KIKUU Reviewed by safina radio on April 23, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.