BOMU LENYE KILO 500 LA ENZI YA VITA VIKUU VYA DUNIA LAPANGWA KUTEGULIWA.


Watu wanatarajiwa kuhamishwa leo katika sehemu kubwa ya katikati ya mji mkuu wa Ujerumani Berlin huku wataalamu wakijiandaa kutungua bomu la enzi ya vita vikuu vya pili vya dunia lenye uzito wa kilo 500 ambalo limegunduliwa wakati wa shughuli za ujenzi.
Image result for bomu la kilo 500 ujerumani
Usafiri unatarajiwa kusitishwa huku zaidi ya watu elfu kumi wakiondolewa kutoka katika maeneo hayo umbali wa mita 800 kutoka mahali bomu lilipo, kikiwemo kituo kikubwa cha treni cha Berlin.
Shirika la usafiri wa treni Ujerumani Deutsche Bahn limesema treni hazitaruhusiwa kusimama katika kituo hicho kuanzia saa nne na usafiri wa treni utasitishwa kabisa kuanzia saa tano na nusu hadi saa saba mchana kwa saa za ukanda huo.
Polisi wamesema bomu litatunguliwa saa tano na nusu lakini huenda shughuli hiyo ikacheleweshwa hadi saa sita kamili.
Safari za ndege hazitarajiwi kukatizwa, ingawa usafiri wa umma kuelekea uwanja wa ndege utaathirika.

BOMU LENYE KILO 500 LA ENZI YA VITA VIKUU VYA DUNIA LAPANGWA KUTEGULIWA. BOMU LENYE KILO 500 LA ENZI YA VITA VIKUU VYA DUNIA LAPANGWA KUTEGULIWA. Reviewed by safina radio on April 20, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.