RAIS MAGUFULI LEO AMEWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI WAKIWEMO MAJAJI 10


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mh. Dk. John Magufuli leo amewaapisha viongozi mbali mbali aliyowateua wiki iliyopita wakiwemo majaji 10 wa mahakama kuu ya Tanzania.

Image result for PICHA YA RAIS MAGUFULI IKULU LEO
RAIS MAGUFULI.

Hafla ya  kuapishwa kwa viongozi hao imefanyika Ikulu jijini Dar es salaam ambapo viongozi walioapishwa ni pamoja na majaji 10 wa mahakama kuu, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Naibu Wakili Mkuu wa Serikali na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

Aidha Rais Magufuli amewaasa Majaji hao kumtanguliza Mungu mbele pamoja na Tanzania ili kuamua mashauri kwa weledi huku akidokeza kuwa kwa sasa Tanzania ipo katika vita vya kiuchumi.

Akizungumza katika hafla hiyo Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi amesema kuwa kazi ya kuhukumu si kazi ya  kuikimbilia bali kuweka uaminifu pamoja na kutenda haki katika kutoa maauzi yao bila upendeleo.

Naye Jaji Mkuu wa Tanzania Ibrahim Juma amesema kuwa mzigo wa kusikiliza mashauri umepungua kutoka mashauri 535 hadi 460 kwa mwaka huku wastani wa kusikiliza mashauri kwa jaji mmoja kwa mwaka ikiwa ni mashauri 178 lakini ambapo wastani uliowekwa na mahakama kwa sasa ya kusikiliza mashauri kwa jaji mmoja kwa mwaka ni mashauri 220.

Kwa upande wake Kamishna wa Maadili kwa Watumishi wa Umma Jaji Mstaafu Harold Nsekela amewaasa majaji hao wapya kuzingatia maadili na kuwaepuka marafiki wabaya na kuepuka upendeleo katika utendaji wao kazi.


RAIS MAGUFULI LEO AMEWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI WAKIWEMO MAJAJI 10 RAIS MAGUFULI LEO  AMEWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI WAKIWEMO MAJAJI 10 Reviewed by safina radio on April 20, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.