WAPALESTINA WATATU WAUAWA KATIKA ENEO LA UKANDA WAGAZA BAADA YA KUFYATULIWA RISASI NA WANAJESHI.
Wanajeshi wa Israel wamefyatua risasi na kuwaua
wapalestina watatu katika matukio mawili tofauti yaliyofanyika mpakani mwa
ukanda wa Gaza na Israel jana Jumapili.
Wanajeshi wa Israel wakiwafyatulia risasi. |
Jeshi la Israel limesema wanajeshi walilazimika
kuwafyatulia risasi baada ya wapalestina hao kuvuka uzio na kuingia maeneo ya
Israel na kuvirushia milipuko vikosi vya Israel.
Tukio la jana Jumapili ni la hivi karibuni
mpakani tangu maandamano dhidi ya Israel yalipoanza tena kwenye ukanda wa Gaza
mnamo Machi 30.
Hata hivyo Wapalestina kadhaa wameuawa na maelfu
wengine kujeruhiwa kutokana na vurugu ambazo zimekuwa zikifanyika maeneo hayo.
WAPALESTINA WATATU WAUAWA KATIKA ENEO LA UKANDA WAGAZA BAADA YA KUFYATULIWA RISASI NA WANAJESHI.
Reviewed by safina radio
on
April 30, 2018
Rating:
No comments