WABUNGE 500 WA EU WAIIONNYA MAREKANI.


Wabunge wapatao 500 kutoka Uingereza, Ufaransa na Ujerumani wamelionya bunge la Marekani, Congress, kuhusu kuvurugika kwa uaminifu katika mahusiano kati ya mataifa ya Ulaya na Marekani na kuendelea kwa mzozo wa Mashariki ya Kati iwapo Marekani itajiondoa katika mkataba wa nyuklia na Iran.
Image result for MABUNGE YA UINGEREZA, UFARANSA NA UJERUMANI.
Wabunge hao wamelihimiza bunge kuunga mkono mkataba huo ambao Rais Donald Trump wa Marekani ametishia kuachana nao.
Utawala wa Trump umetaka mkataba huo wa nyuklia ulioafikiwa 2015 ufanyiwe marekebisho kufikia tarehe 12 Mei mwaka huu, vinginevyo Marekani itaiwekea vikwazo Iran na kuusambaratisha mkataba huo licha ya Iran kuuheshimu.
Hata hivyo Wabunge kutoka nchi hizo tatu ambazo ni miongoni mwa nchi zilizoridhia mkataba na Iran wameonya kuwa Marekani kuachana na mkataba huho heunda kukafikisha mwisho hatua zilizowekwa za kuudhibiti mpango wa nyuklia wa Iran na kusababisha chanzo cha mzozo Mashariki ya Kati.

WABUNGE 500 WA EU WAIIONNYA MAREKANI. WABUNGE 500 WA EU WAIIONNYA MAREKANI. Reviewed by safina radio on April 20, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.