MATUMIZI YA SILAHA ZA SUMU NCHINI SYRIA UNASTAHILI UCHUNGUZI.


Baada ya mkutano wake wa kilele nchi zote zilizoko katika Jumuiya ya Mataifa ya Kiarabu isipokuwa Syria na Qatar, zimesema uhalifu wa matumzi ya silaha za sumu na serikali ya Syria unastahili kuchunguzwa.

Image result for PICHA YA SHAMBULIZI NCHINI SYRIA


Jumuiya hiyo pia imeilaani Iran kwa kutotambua uhuru wa nchi zingine. Katika hotuba ya ufunguzi ya  Mfalme Salman wa Saudi Arabia ameikosoa hatua ya wazi ya Iran ya kuingilia masuala ya nchi zingine.

Iran ni mwandamani wa rais wa Syria Bashar al-Assad na imekuwa ikichochea vita nchini Yemen dhidi ya Saudi Arabia.

Mkutano huo wa kilele umefanyika Saudi Arabia na umeunga mkono kushambuliwa kwa sehemu zenye silaha za Syria kulikofanywa na Marekani, Uingereza na Ufaransa.

Lakini wanachama wengine wa Jumuiya hiyo kama Iraq na Lebanon walikuwa wamelaani mashambulizi hayo.

 Licha ya kuwa rafiki mkubwa wa Marekani Mfalme Salman pia amemshambulia Rais Donald Trump kwa kuitambua Jerusalem kama mji mkuu wa Israel.

MATUMIZI YA SILAHA ZA SUMU NCHINI SYRIA UNASTAHILI UCHUNGUZI. MATUMIZI YA SILAHA ZA SUMU NCHINI SYRIA UNASTAHILI UCHUNGUZI. Reviewed by safina radio on April 16, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.