TANZANIA INATAMBUA MCHANGO WA UINGEREZA KATIKA KUZUIA UJANGILI WA WANYAMAPORI.


Makamu wa rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Samia Suluhu Hassan amesema kuwa Tanznaia inatambua mchango wa Uingereza katika kuzuia ujangili wa wanyama pori hapa nchini.

Image result for Makamu wa rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Samia Suluhu Hassan
Makamu wa Rais Samia Suluhu.

Mh Suluhu ameyasema hayo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Mwanamfalme Price Williams katika jumba la kifalme lililopo mjini London nchini Uingereza.

Amesema kuwa serikali ya Tanzania imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kupambana na kuzuia majangili ingawa bado haijawa na tekinolojia yenye uwezo ya kuona wanyama wote lakini wanaendea kuimarisha ulinzi wa wanyama hao.

Kwa upande wake Price William amemuahidi makamu wa rais kuisaidia Tanzania katika ulinzi wa wanyama pori kwa kutumia tekinolojia ya hali ya juu,ambapo pia amemkaribisha rais Magufuli katika mkutano wa kuwalinda wanyama pori unaotarajiwa kufanyika mwezi Octoba mwaka huu mjini London.

Hata hivyo Makamu wa rais yuko mjini Uingereza kumwakilisha rais Magufuli katika mkutano wa wakuu wa nchi za jumuiya ya madola.

TANZANIA INATAMBUA MCHANGO WA UINGEREZA KATIKA KUZUIA UJANGILI WA WANYAMAPORI. TANZANIA INATAMBUA MCHANGO WA UINGEREZA KATIKA KUZUIA UJANGILI WA WANYAMAPORI. Reviewed by safina radio on April 17, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.