JESHI LA POLISI MKOANI MANYARA LINAENDELEA KUFANYA UCHUNGUZI KUBAINI WANAOHAMASISHA MAANDAMANO.


Jeshi la Polisi Mkoani Manyara limesema kuwa linaendelea kufanya uchunguzi ili kuwabaini wananchi wanaohamasisha maandamano yasiyo halali kwa njia ya mtandao April 26 mwaka huu hapa nchini.

Image result for PICHA YA AUGUSTINO SENGA KAMANDA WA POLISI MKOANI MANYARA
KAMANDA WA POLISI MKOANI MANYARA AUGUSTINO SENGA.
Hayo yamesemwa na kamanda wa jeshi la polisi mkoani Manyara kamishna msaidizi wa polisi Augustino Senga wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juu ya namna jeshi hilo lilivyojipanga kupambana na waalifu wanaotaka kuleta uvunjifu wa amani mkoani humo.

Kamanda Senga amesema kuwa katika mkoa wa Manyara kumekuwa na taarifa za maandamano hivyo kwa sasa wanaendelea na uchunguzi ili kuwabaini wale ambao wanaohamasisha maandamano hayo ili waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Amewataka wananchi kuelewa kuwa maandamano hayo ni kinyume cha sheria kwa kuwa hayana kibali hivyo wasikubali kufuata mkumbo na kutumika vibaya na watu wasiolitakia mema Taifa la Tanzania.

Hata hivyo amewataka wanasiasa kufanya siasa za kistaarabu ambazo hazivunji usalama,hakiwala amani ambao utaweza kuathiri maisha ya watu na mali zao.


JESHI LA POLISI MKOANI MANYARA LINAENDELEA KUFANYA UCHUNGUZI KUBAINI WANAOHAMASISHA MAANDAMANO. JESHI  LA POLISI MKOANI MANYARA LINAENDELEA KUFANYA UCHUNGUZI  KUBAINI WANAOHAMASISHA MAANDAMANO. Reviewed by safina radio on April 20, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.