RAIS WA AFRIKA YA KUSINI CYRIL RAMAPHOSA AMESITISHA ZIARA YAKE NCHINI UINGEREZA


Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amelazimika kusitisha ziara yake nchini Uingereza anakohudhuria mkutano wa viongozi kutoka mataifa ya Jumuiya ya Madola ili kurejea nyumbani kutokana na machafuko yanayoshuhudiwa Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo.
Image result for PICHA YA CYRIL RAMAPHOSA
RAIS WA AFRIKA YA KUSINI CYRIL RAMAPHOSA
Wakaazi wa mkoa huo wamekuwa wakiandamana, na kupora mali za wafanyibiashara hasa kutoka nje ya nchi hiyo kwa madai ya kuwa wanataka ajira, makaazi bora na kumalizwa kwa ufisadi.
Shughuli zimekwama katika mji mkuu wa mkoa wa Mahikeng, huku maduka yakisalia kufungwa na waandamanaji kuteketeza kwa moto matairi barabarani wakitaka pia kujiuzulu kwa viongozi wa mkoa huo.
Rais Ramaphosa anarejea nyumbani kujaribu kumaliza machafuko hayo ambayo yameelezwa na kiongozi wa eneo hilo Supra Mahumapelo kuwa yamechochewa kisiasa.
Hata hivyo Kuporwa kwa mali na uharibu unatokea ni pigo kwa serikali ya rais Ramaphosa ambaye wiki hii, ametumia muda mwingi akiwa jijini London kuwashawishi wawekezaji kuja kuwekeza nchini humo.


RAIS WA AFRIKA YA KUSINI CYRIL RAMAPHOSA AMESITISHA ZIARA YAKE NCHINI UINGEREZA RAIS WA AFRIKA YA KUSINI CYRIL RAMAPHOSA AMESITISHA ZIARA YAKE NCHINI UINGEREZA Reviewed by safina radio on April 20, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.