TANAPA YAHAKIKISHA INAREJESHI MAWAILIANO YA MIUNDOMBINU YA BARABARA NDANI YA HIFADHI YA ZIWA MANYARA.


Hali ya miundombinu katika hifadhi ya ziwa manyara iliyoharibiwa na mvua hususani daraja la Marera imerejea kufuatia jitihada zilizofanywa na Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Nchini TANAPA.

Image result for Meneja wa Mawasiliano wa TANAPA Paskali Shelutete
Meneja wa Mawasiliano wa TANAPA Paskali Shelutete.
Meneja wa Mawasiliano wa TANAPA Paskali Shelutete amesema kuwa miundombinu katika hifadhi hiyo iliharibiwa pakubwa na maji ya mvua na kusababisha vivutio vya utalii kutokufikika kwa urahisi.

Aidha, amesema kuwa wamefanya mazungumzo na wadau wa utalii ambao ni wageni wanaofika katika maeneo hayo ambapo wamewataka wasitishe ratiba za safari zao za utalii kwa muda ili Mamlaka iweze kurejesha hali ya miundombinu iliyoharibika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Hata hivyo amewatoa wasiwasi wadau hao wa utalii wanaopenda kuitembelea hifadhi  hiyo kwa kuwa Mamlaka ya hifadhi za taifa imeimarisha vikosi vya dharura kwa lengo la kuhakikisha kuwa miundombinu inaendelea kupitika hasa kipindi hiki cha mvua.

TANAPA YAHAKIKISHA INAREJESHI MAWAILIANO YA MIUNDOMBINU YA BARABARA NDANI YA HIFADHI YA ZIWA MANYARA. TANAPA YAHAKIKISHA INAREJESHI MAWAILIANO YA MIUNDOMBINU YA BARABARA NDANI YA HIFADHI YA ZIWA MANYARA. Reviewed by safina radio on April 18, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.