WAMILIKI WA VITUO VYA WATOTO YATIMA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA
TAREHE 28-11-2017
Wamiliki
wanaoendesha vituo vya kuwalea watoto yatima na wanaoishi katika mazingira
magumu hapa nchini wametakiwa kufuata sheria za uanzishwaji wa vituo hivyo
ikiwemo kuvisajili na kutoa huduma bora kwa watoto hao.
Kauli hiyo
imetolewa na afisa ustawi wa jamii kutoka halmashauri ya Meru Bi Restuta Mvungi
wakati akizungumza na Redio Safina kuhusu huduma zinazotakiwa kutolewa katika vituo mbalimbali
vinavyotunza watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu.
Bi Mvungi amesema
kuwa baadhi ya huduma zinazotakiwa kutolewa na vituo hivyo ni pamoja na kuwa na
nyumba nzuri,matibabu,malazi pamoja na lishe bora,na vituo ambavyo vinakiuka
taratibu hizo vinachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kuvifungia.
Amesema kuwa katika
halmashauri ya Meru kuna vituo 30 na wao kama watu wa ustawi wa jamii wamekuwa
wakitoa elimu kwa vituo hivyo ili wajue wajibu wao katika kuwahudumia watoto
hao kama sheria ya mtoto inavyoelekeza.
Hata hivyo afisa
huyo amewaonya wale wote wanaotumia vituo vya kuwalea watoto yatima
kujinufaisha wenyewe na watakaobainika watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.
WAMILIKI WA VITUO VYA WATOTO YATIMA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA
Reviewed by safina radio
on
November 28, 2017
Rating:

No comments