WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI MH. LUHAGA MPINA AMEWATAKA WANANCHI MKOANI KAGERA KUANZISHA MIRADI YA UFUGAJI SAMAKI.
2-11-2017
Waziri wa Mifugo na
Uvuvi Mh Luhaga Mpina amewataka wananchi Mkoani Kagera kuanzisha miradi ya
ufugaji wa samaki ili kuondoa changamoto ya upatikanaji wa bidhaa hiyo.
Akizungumza mkoani humo
alipotembelea kiwanda cha kuchakata minofu ya samaki cha VIC Waziri Mpina
amesema upatikanaji wa samaki umekuwa mdogo kutokana na wananchi kutotilia
manani katika uzalishaji wa samaki.
Aidha, Waziri Mpina
amemuagiza mwekezaji wa kiwanda hicho kuhakikisha kuwa ndani ya mwaka mmoja
kiwanda chake kiwe kinazalisha tani sitini za uwezo wa uzalishaji wake wa
minofu hiyo.
Hata hivyo, amekitaka
kiwanda hicho kuongeza uzalishaji kutoka tani kumi na saba za sasa hadi kufikia
tani ishirini na tano.
WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI MH. LUHAGA MPINA AMEWATAKA WANANCHI MKOANI KAGERA KUANZISHA MIRADI YA UFUGAJI SAMAKI.
Reviewed by safina radio
on
November 02, 2017
Rating:

No comments