HALMASHAURI ZOTE HAPA NCHINI ZATAKIWA KUSHIRIKIANA NA WADAU WA ELIMU ILI KUKAMILISHA UJENZI WA MAABARA
TAREHE 10-11-2017
Naibu waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa Mh Joseph Kakunda amezitaka halmashauri zote hapa nchini kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu ili kukamilisha ujenzi wa maabara za sekondari zinazotakiwa katika maeneo yao.
Naibu waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa Mh Joseph Kakunda amezitaka halmashauri zote hapa nchini kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu ili kukamilisha ujenzi wa maabara za sekondari zinazotakiwa katika maeneo yao.
Mh Kakunda ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati
akijibu maswali ya wabunge bungeni waliotaka kujua serikali imefikia wapi
katika kutekeleza mpango wake wa ujenzi wa maabara,ambapo amesema kuwa kati ya
maabara elfu kumi mia tatu thelathini na saba zinazohitajika hapa nchini tayari
maabara elfu sita mia mbili themanini na saba sawa na asilimia 60.7
zimeshakamilika.
Ameongeza kuwa ili
maabara hizo zikamilike kwa wakati ni vyema halmshauri zote hapa nchini zikashirikiana
na wadau mbalimbali wa maendeleo kukamilisha ujenzi wa maabara hizo zilizobaki ili
kuboresha mazingira bora ya kujisomea kwa wananfunzi.
Aidha katika hatua
nyingine waziri huyo amesema kuwa katika siku za mbeleni serikali ina mpango wa
kutumia sera mpya ya elimu ya mwaka wa 2014 itakayomlazimisha mtoto mwenye umri
wa kwenda shule kusoma chekechea mwaka mmoja,msingi miaka 6 na sekondari miaka
4 ili apate cheti cha kuhitimu cha Leaving Certicate.
HALMASHAURI ZOTE HAPA NCHINI ZATAKIWA KUSHIRIKIANA NA WADAU WA ELIMU ILI KUKAMILISHA UJENZI WA MAABARA
Reviewed by safina radio
on
November 10, 2017
Rating:
No comments