MUGABE AJIUZULU WANANCHI WASHEREKEA

22-11-2017

Barua ya kujiuzulu kwake iliyosomwa bungeni na Spika Jacob Mudenda, ilisema Mugabe amefanya hivyo kwa mujibu wa katiba, na kwa kuzingatia maslahi ya nchi na ubadilishanaji madaraka kwa njia ya amani.

Sherehe hizo zilizoanzia katika chumba walimokuwa wakikutana wabunge zilienea katika mitaa ya mji mkuu Harare na nchini kote.

 Chama tawala cha ZANU-PF ambacho tayari kilikuwa kimeanzisha mchakato wa kumtimua Mugabe, kimesema aliyekuwa makamu wa rais Emmerson Mnangagwa ataapishwa hivi karibuni kuwa rais wa mpito hadi uchaguzi mkuu utakapofanyika mwakani.


Robert Mugabe mwenye umri wa miaka 93 ameitawala Zimbabwe tangu ilipopata uhuru wake miaka 37 iliyopita, lakini azma yake ya kumrithisha madaraka mkewe Grace yamesababisha uingiliaji wa jeshi, ambao umemshinikiza kujiuzulu.
MUGABE AJIUZULU WANANCHI WASHEREKEA MUGABE AJIUZULU WANANCHI WASHEREKEA Reviewed by safina radio on November 22, 2017 Rating: 5

No comments