KANISA LASHAMBULIWA MAREKANI NA WATU 26 KUUAWA
TAREHE 06-11-2017
Maafisa polisi nchini Marekani wamesema kuwa Watu 26
wameuawa na wengine 20 wamejeruhiwa
vibaya kwa kupigwa risasi na mtu mwenye silaha
aliyewafyatulia risasi waumini katika kanisa moja jimbo la Texas wakati wa
ibada.
Shambulio hilo limetekelezwa
katika kanisa la First Baptist Church katika mji wa Sutherland Springs, mji
mdogo katika wilaya ya Wilson, Texas.
Mshambuliaji, ambaye
anadaiwa kuuawa baada ya kutekeleza mauaji hayo, aliingia kanisani na kuanza
kuwafyatulia risasi watu mwendo wa saa tano nusu asubuhi.
Gavana wa Texas Greg Abbott amethibitisha idadi ya waliofariki na
kusema ndicho kisa kibaya zaidi cha mauaji ya kutekelezwa kwa kutumia bunduki
katika historia ya Texas.
Mshukiwa ametajwa kuwa ni mwanamume mzungu wa umri wa
miaka 20 ambaye alikuwa amevalia mavazi meusi na fulana ya kujikinga dhidi ya
risasi pamoja na kuwa na bunduki yenye uwezo mkubwa.
Hata hivyo Mhubiri wa kanisa hilo la
First Baptist Frank
Pomeroy, amesema kwamba binti yake wa miaka 14 kwa jina Annabelle ni
miongoni mwa waliouawa, ambapo Maafisa wa FBI kutoka San Antonio wametumwa
kufanya uchunguzi lakini kufikia sasa lengo la mshambuliaji halijabainika.
KANISA LASHAMBULIWA MAREKANI NA WATU 26 KUUAWA
Reviewed by safina radio
on
November 06, 2017
Rating:

No comments