SERIKALI KUPITIA WIZARA YA MAMBO YA NDANI IMESEMA INASHIRIKIANA NA MAKAMPUNI BINAFSI YA ULINZI ILI KUAJIRI WAFANYAKAZI WASIOKUWA NA HISTORIA YA UHALIFU

TAREHE 13-11-2017


Serikali kupitia wizara ya mambo ya ndani ya nchi imesema kuwa imekuwa ikishirikiana na makampuni binafsi ya ulinzi ili kuhakikisha kuwa wafanyakazi wanaoajiriwa katika makampuni hayo hawana historia za kiuhalifu.

Hayo yameelezwa leo bungeni mjini Dodoma na naibu waziri wa ofisi ya waziri mkuu sera,bunge,ajira,vijana na watu wenye ulemavu Mh Antony Mavunde wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalumu Mh Ruth Mollel aliyetaka kujua ni kwa jinsi gani serikali inasimamia makampuni binafsi ya ulinzi ili kuhakikisha kuwa wale wote walioajiriwa katika makampuni hayo hawana historia za kiuhalifu.

Mh Mavunde amesema kuwa ushirikiano wa serikali pamoja na makampuni hayo unaazia kwenye usajili baada ya kupitia na kutathimini maombi ya kuanzishwa kwa kampuni husika ambapo kazi hiyo hufanywa na jeshi la polisi kwa kushirikiana na wakala wa usajili wa makampuni hapa nchini (BRELA).

Ameongeza kuwa  serikali inafahamu mchango mkubwa unaotolewa na makampuni ya ulinzi hapa nchini katika kusaidia jeshi la polisi kulinda usalama wa wananchi na mali zao kwa kuwa polisi walioko hawatoshi kwa polisi mmoja analazimika kuwalinda watu zaidi ya elfu moja badala ya watu mia nne na hamsini.


Hata hivyo amesema jeshi la polisi litaenedelea kutoa mafunzo kwa makampuni binafsi ya ulinzi,kutoa vitambulisho pamoja na kutoa ushauri ili kuboresha na kuhakikisha huduma ya ulinzi inatolewa katika viwango vinavyotakiwa.
SERIKALI KUPITIA WIZARA YA MAMBO YA NDANI IMESEMA INASHIRIKIANA NA MAKAMPUNI BINAFSI YA ULINZI ILI KUAJIRI WAFANYAKAZI WASIOKUWA NA HISTORIA YA UHALIFU SERIKALI  KUPITIA  WIZARA YA MAMBO YA NDANI  IMESEMA  INASHIRIKIANA  NA MAKAMPUNI   BINAFSI YA ULINZI  ILI KUAJIRI WAFANYAKAZI  WASIOKUWA NA HISTORIA YA UHALIFU Reviewed by safina radio on November 13, 2017 Rating: 5

No comments