RAIS MPYA WA ZIMBABWE EMMERSON MNANGAGWA ATOA MIEZI 3 KWA WALIOPORA MALI ZA UMA

TAREHE 28-11-2017


Rais mpya wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa ametoa muda wa miezi mitatu kwa wale wote waliopora fedha za umma na kuzificha nje ya nchi kuzirejesha.

Katika taarifa iliyotolewa jana Jumanne, Mnangagwa amesema muda huo ukimalizika Februari mwakani, serikali itawakamata na kuwafikisha mahakamani wale wote ambao hawatakuwa wameitii amri hiyo.

Hayo yanajiri wakati ambao aliyekuwa waziri wa fedha wa Zimbabwe, Ignatius Chombo ambaye alikuwa amekamatwa na jeshi baada ya kuchukua mamlaka, akifikishwa mahakamani Ijumaa iliyopita akikabiliwa na tuhuma za ufisadi.

Kwa mujibu wa wakili wake, waziri huyo wa zamani wa fedha wa Zimbabwe anakabiliwa na mashtaka ya ufisadi na utumiaji mbaya wa madaraka wakati alipokuwa waziri wa serikali za mitaa. 

Ignatius Chombo ni miongoni mwa maafisa wakuu wa serikali ya Zimbabwe waliokamatwa baada ya Robert Mugabe kuzuiliwa nyumbani kwake mnamo tarehe 14 Novemba mwaka huu.
RAIS MPYA WA ZIMBABWE EMMERSON MNANGAGWA ATOA MIEZI 3 KWA WALIOPORA MALI ZA UMA RAIS MPYA WA ZIMBABWE EMMERSON  MNANGAGWA  ATOA MIEZI 3 KWA WALIOPORA MALI ZA UMA Reviewed by safina radio on November 29, 2017 Rating: 5

No comments