KIMBUNGA CHAUA WATU 27 HUKO VIETNAM
TAREHE 06-11-2017
Kimbunga Damrey kimepiga maeneo ya
kusini na kati ya Vietnam na kusababisha vifo vya watu 27, na wengine zaidi ya
20 hawajulikani waliko.
Kimbunga hicho kilifika
maeneo ya bara kikiwa na upepo unaovuma
kwa kasi ya kilomita 90 kwa saa, ambapo Nyumba zaidi ya elfu arobaini zimeharibiwa vibaya na maelfu ya watu
wamehamishwa makwao, na Maeneo mengi yakiwa hayana umeme.
Hata hivyo Eneo
lililoathiriwa zaidi ni jiji la Nha Trang lililopo umbali wa kilomita mia tano kusini mwa jiji la Da Nang, katika pwani ya nchi hiyo ambapo
viongozi wa mataifa wanachama wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Asia na Pasific (Apec) wanatarajiwa
kuhudhuria mkutano mkuu baadaye wiki hii.
KIMBUNGA CHAUA WATU 27 HUKO VIETNAM
Reviewed by safina radio
on
November 06, 2017
Rating:

No comments