RAIS MUGABE AMESISITIZA KUWA YEYE NDIE KIONGOZI HALALI WA ZIMBABWE
TAREHE 17-11-2017
Rais Robert Mugabe
anasisitiza kuwa yeye ndiye kiongozi halali wa Zimbabwe na hataki kushiriki
mazungumzo yanayofanywa na Kasisi mmoja wa Kikatoliki ya kumuezesha rais huyo
mwenye umri wa miaka 93 kuondoka madarakani kwa amani baada ya mapinduzi ya
kijeshi.
Habari kutoka kwa washirika wa ngazi ya juu waliowekwa katika
kizuizi cha nyumbani pamoja na Mugabe na mkewe, Grace, nyumbani kwa kiongozi
huyo mjini Harare, imesema Mugabe hana mipango ya kujiuzulu kwa hiari kabla ya
uchaguzi uliopangwa kufanyika mwaka
ujao.
Upinzani nchini humo umemtaka Mugabe ajiuzulu
maramoja na kuundwa haraka serikali ya mpito.
Katibu Mkuu wa
chama cha MDC-T chake Morgan Tsvangirai amesema wanaunga mkono hatua ya jeshi
lakini nchi inapaswa kurejeshwa haraka katika uongozi wa kikatiba.
Wajumbe maalumu
waliotumwa na Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma wanafany amazungumzo kuhusu
hatima ya Mugabe na viongozi wa Zimbabwe.
RAIS MUGABE AMESISITIZA KUWA YEYE NDIE KIONGOZI HALALI WA ZIMBABWE
Reviewed by safina radio
on
November 17, 2017
Rating:

No comments