WAZIRI MKUU MH. MAJALIWA AMWAGIZA SIRRO KUWAKAMATA BW. BAHAMAN WA KAMPUNI YA NAS KWA KUTAKA KUTOA MAGARI BANDARINI KWA KUTUMIA JINA LA WAZIRI MKUU

TAREHE 29-11-2017


Waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh Majaliwa Kassimu Majaliwa amemtaka mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Saimon Sirro kuwakamata Bw Bahaman wa kampuni NAS na wakala wa kampuni ya WOMAC SAMWEL kwa kutaka kutoa bandarini magari makubwa aina ya Semtrella 44 kwa kutumia jina la waziri mkuu.

Mh Majaliwa ametoa agizo hilo alipofanya  ziara ya kushtukiza katika bandari ya Dar-es-salaam baada ya kupata taarifa za mfanyabiashara huyo kutaka kutapeli uongozi wa bandari kwa kutak akutoa magari hayo yaliyoingizwa hapa nchini mwaka 2015 kutoka nchini Uturuki.

Aidha waziri mkuu ameitaka mamlaka ya usimamizi wa bandari hapa nchini TPA kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na kutowasikiliza wafanyabiashara wanaotaka kukwepa kodi madai ya kupewa vibali vya msamaha wa kodi kutoka kwa viongozi wa juu serikalini.

Amesema kuwa serikali ya awamu ya tano imekuwa ikisimamia ukusanyaji wa mapato,hivyo haitawavumilia wafanyabiashara wanaotumia majina wa viongozi wakubwa hapa nchini ikiwemo jina la rais kuingiza bidhaa zao bila kulipa mapato ya serikali kwa maendeleo ya watanzania wote.


Hata hivyo ziara ya waziri mkuu imekuja siku chache baada ya rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh John Magufuli kufanya ziara nyingine ya kushtukiza bandarini hapo na kugundua kuwepo kwa  magari 53 ya wagonjwa  yaliyoingizwa hapa nchini mwaka wa 2015 bila mmiliki wake kujulikana.
WAZIRI MKUU MH. MAJALIWA AMWAGIZA SIRRO KUWAKAMATA BW. BAHAMAN WA KAMPUNI YA NAS KWA KUTAKA KUTOA MAGARI BANDARINI KWA KUTUMIA JINA LA WAZIRI MKUU WAZIRI MKUU MH. MAJALIWA AMWAGIZA SIRRO  KUWAKAMATA BW. BAHAMAN WA KAMPUNI YA NAS KWA KUTAKA KUTOA MAGARI BANDARINI KWA KUTUMIA JINA LA WAZIRI MKUU Reviewed by safina radio on November 29, 2017 Rating: 5

No comments