WAZIRI WA AFYA MH. UMMY MWALIMU AMEWATAKA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII NCHINI KUTAMBUA NAFASI ZAO
TAREHE 07-11-2017
Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewataka Maafisa
maendeleo ya jamii nchini kutambua nafasi zao katika kuamsha ari ya wananchi
kushiriki katika uchumi wa Viwanda.
Waziri Ummy ametoa
kauli hiyo Mjini Dodoma wakati akifungua mkutano wa 12 wa sekta ya maendeleo ya
jamii ambapo ameutumia mkutano huo kuwataka maafisa hao wa maendeleo ya jamii
kuji tathmini kiutendaji na kufanya mabadiliko ya kiutendaji ili kuamsha ari ya
wananchi katika kushiriki uchumi wa viwanda.
Aidha, Waziri Mwalimu
amesema kuwa Wizara ilifanya tathmini ya mchango wa sekta ya maendeleo ya jamii
kwa miaka hamsini ya Muungano na kubaini kuwa ari ya wananchi ya kuchangia
maendeleo kwa sasa imeshuka ikilinganishwa na miaka ya 1960 hadi 1970.
Mbali na hayo ameongeza
kuwa mitaala ya vyuo vinavyofundisha taaluma ya maendeleo ya jamii ni lazima
itazamwe upya kama inaakisi maendeleo ya karne ya 21 sambamba na kutazama
majukumu ya maafisa hao ngazi ya Wilaya na Mkoa kama yanaendana na matarajio ya serikali ya awamu ya tano.
WAZIRI WA AFYA MH. UMMY MWALIMU AMEWATAKA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII NCHINI KUTAMBUA NAFASI ZAO
Reviewed by safina radio
on
November 07, 2017
Rating:

No comments