IMEELEZWA KUWA CHANZO CHA ONGEZEKO LA WATOTO YATIMA NA WANAOISHI KWENYE MAZINGIRA MAGUMU NI KUKOSA MALEZI BORA YA WAZAZI.
TAREHE 06-11-2017
Imeelezwa kuwa chanzo kimojawapo kinachosababisha
ongezeko la watoto yatima pamoja na wanaoishi katika mazingira magumu hapa
nchini ni baada ya kukosa malezi bora kutoka
kwa wazazi wao.
Hayo yameelezwa na afisa ustawi wa jamii wilaya ya
Arumeru Bi Restusta Mvungi wakati akizungumza na Redio Safina kuhusu haki
mbalimbali za watoto pamoja na athari wanazokutana nazo baada ya wazazi wawili
kutengana katika familia.
Amesema kuwa katika shughuli zao za ustawi wa jamii
wamebaini kuwa watoto wengi yatima pamoja na wanaoishi katika mazingira magumu wana
matatizo ya kifamilia hasa baada ya wanandoa kutengana,ambapo mbali na kuishi
katika mazingira hayo pia wanaathirika kisaikolojia na kujiona hawana thamani
katika jamii.
Ameongeza kwamba ili kukabiliana na changamoto hiyo
wao kama watu wanaoshughulika na ustawi wa jamii wamekuwa wakitoa elimu kwa
jamii kuhusu umuhimu wa kuwalea watoto wakati wazazi wakiwa wawili na namna ya
kusuhisha matatizo yao pale wanapohitilafiana.
Hata hivyo ofisi za ustawi wa jamii hapa nchini hufanya
shughuli mbalimbali ikiwemo kuwahudumia watoto wanaoishi katika mazingira
hatarishi,haki za watoto pamoja na watu
wenye ulemavu na wazee.
IMEELEZWA KUWA CHANZO CHA ONGEZEKO LA WATOTO YATIMA NA WANAOISHI KWENYE MAZINGIRA MAGUMU NI KUKOSA MALEZI BORA YA WAZAZI.
Reviewed by safina radio
on
November 06, 2017
Rating:

No comments