TAKRIBANI WATU 200 WAFARIKI KATIKA TETEMEKO LA ARDHI HUKO IRAN




TAREHE 13-11-2017
Takriban watu 200 wameuawa baada ya tetemeko lenye ukubwa wa kipimo cha Richa cha 7.3 lililotokea katika mkoa ulio magharibi mwa Iran wa Kermanshah.
Kulingana na kituo cha Marekani USGS tetekemo hilo lilitokea umbali wa kilomita 33.9 chini ya ardhi na lilisikika nchini Uturuki, Israel na Kuwait
Wengi wa waathiriwa walikuwa katika mji wa Sarpol-e Zahab, kilomita 15 kutoka mpakani na kutoka kilometa 30 kusini magharibi mwa mji wa Halabja karibu na mpaka wa Iran..

Kwa mujibu wa afisa wa shirika la msalaba mwekundu nchini Iran, Morteza Salim amesema kuwa uharibifu umeripotiwa kutokea katika vijiji vinane na baadhi ya vijiji vimekumbwa na matatizo ya nguvu za umeme na mawasiliano yamevurugwa.
TAKRIBANI WATU 200 WAFARIKI KATIKA TETEMEKO LA ARDHI HUKO IRAN TAKRIBANI WATU 200 WAFARIKI KATIKA TETEMEKO LA ARDHI HUKO IRAN Reviewed by safina radio on November 13, 2017 Rating: 5

No comments