WAZIRI WA SHERIA PROFESA PALAMAGAMBA KABUDI AMEKUTANA NA NAIBU WAZIRI WA SHERIA WA CHINA ZAO DA CHING.
TAREHE 30-11-2017
Waziri wa
Katiba na Sheria Profesa. Palamagamba Kabudi amekutana na Naibu waziri wa
Sheria wa China Zao Da Ching na kujadili masuala mbalimbali ikiwemo kuimarisha
ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na China.
Kikao hicho
kati ya Profesa. Kabudi na Naibu Waziri huyo wa Sheria wa China Bw. Ching na ujumbe
wake umefanyika jijini Dar es salaam,ambapo Katika
kikao hicho Waziri Palamagamba amesema kuwa Tanzania na China itaongeza
ushirikiano wake katika maeneo mengine muhimu ikiwemo Ulinzi na Usalama.
Akizungumzia
ziara ya Naibu Waziri huyo wa Sheria wa China na ujumbe wake, Profesa,Kabudi
amesema kuwa ziara hiyo itafungua milango mipya katika nyanja mbalimbali za
maendeleo.
Hata hivyo naibu
waziri huyo wa Sheria wa China,Disemba Mosi mwaka huu atafanya ziara ya siku moja visiwani Zanzibar
ambapo atakutana na Jaji Mkuu wa Jamuhuri
ya Muungano wa Tanzania Profesa. Ibrahim
Juma na viongozi wengine wa Zanzibar.
WAZIRI WA SHERIA PROFESA PALAMAGAMBA KABUDI AMEKUTANA NA NAIBU WAZIRI WA SHERIA WA CHINA ZAO DA CHING.
Reviewed by safina radio
on
November 30, 2017
Rating:

No comments