WANARIADHA 5 WA URUSI WAFUNGIWA MAISHA
TAREHE 28-11-2017

Wanariadha wengine watano wa Urusi wamefungiwa kushiriki michuano ya kimataifa ya Olimpiki kwa maisha yao yote baada ya kamati ya kimataifa ya Olimpiki kuwabaini kutumia dawa zilizokataliwa michezoni.
Sergei Chudinov, Aleksei Negodailo, Dmitry Trunenkov, Yana Romanova na Olga Vilukhina ndio waliokumbwa na adhabu hiyo.
IOC inasema kufungiwa huko kunatokana na kamati ya 2016 ya McLaren iliyoonyesha watumiaji wa dawa hizo.
Siku ya Jumatatu IOC ilitangaza adhabu hiyo na kuonya kuwa bado itaendelea kwa wale wote watakaojaribu kutumia dawa hizo.
WANARIADHA 5 WA URUSI WAFUNGIWA MAISHA
Reviewed by safina radio
on
November 28, 2017
Rating:
No comments