WAHAMIAJI 50 WAKAMATWA KATIKA MTAA WA BUGANDA KATA YA CHIBULA WILAYANI ILEMELA MKOANI MWANZA.

TAREHE 16-11-2017



Operesheni ya kuwakamata wahamiaji Haramu iliyoanza mwezi Septemba Jijini Mwanza imesaidia kukamata zaidi ya wahamiaji 50 katika Mtaa wa Buganda Kata ya Chibula Wilayani Ilemela Mkoani Mwanza wakiwa katika shughuli za kilimo na uvuvi kwenye mwamabao wa Ziwa Victoria.

Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza Naibu Kamisha Paul Ranga amesema uhamiaji huo haramu umekamatwa Novemba Mwaka huu baada ya Maofisa Uhamiaji kupewa taarifa za siri na baadhi ya wananchi.

Aidha, Afisa huyo wa Uhamiaji wa Mkoa wa Mwanza amesema zoezi hilo la uhakiki wa hati za uhifadhi kwa wageni 297 imebainika wageni 34 hati zao ni feki.

 Kamishna Ranga ameongeza kuwa zaidi ya Wahamiaji haramu 120 kutoka nchi tisa ikiwemo Burundi, Ethiopia, Kenya watafikishwa Mahakamani huku wakitaja sababu za Wahamiaji hao kuja Tanzania ni pamoja na mazingira Magumu nchini kwao.


Vile vile, amesema kuwa mbali na mazingira kuwa magumu ya nchi wanakotoka wahamiaji hao lakini lengo kubwa linalowafanya wahamiaji hao haramu kuja Tanzania ni pamoja na kwenda kuishi Afrika Kusini kutokana na wao kuwasiliana na ndugu zao waliko huko kwa ajili ya kazi hivyo, Tanzania ni kama njia ya Kufikia.
WAHAMIAJI 50 WAKAMATWA KATIKA MTAA WA BUGANDA KATA YA CHIBULA WILAYANI ILEMELA MKOANI MWANZA. WAHAMIAJI  50  WAKAMATWA KATIKA MTAA WA BUGANDA KATA YA CHIBULA WILAYANI ILEMELA MKOANI MWANZA. Reviewed by safina radio on November 16, 2017 Rating: 5

No comments