WAZIRI MKUU WA ISRAEL BENJAMINI NETANYAHU AWAONYA WANAMGAMBO WA GAZA

TAREHE 13-11-2017


Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amewaonya wanamgambo wa Gaza dhidi ya kuishambulia Israel baada ya kundi la jihadi kuapa kulipiza kisasi kutokana na moja ya mahandaki yake kushambuliwa.

Netanyahu amesema leo kuwa Israel itajibu kwa shambulizi kubwa iwapo mtu yeyote atajaribu kuishambulia nchi yake.

Waziri Mkuu huyo ameongeza kuwa Israel inalishutumu kundi la Hamas ambalo linaidhibiti Gaza kuhusika na mashambulizi yaliyoanzishwa kutoka kwenye eneo hilo.

Kundi hilo limeapa kulipiza kisasi baada ya handaki lake lililochimbwa kutoka Gaza hadi Israel, kushambuliwa mwezi uliopita na kuwaua baadhi ya wapiganaji.


Katika matukio kadhaa wapiganaji wa Gaza walifanikiwa kupata taarifa za siri kutoka Israel kupitia handaki hilo wakati wa mapigano ya mwaka uliopita.
WAZIRI MKUU WA ISRAEL BENJAMINI NETANYAHU AWAONYA WANAMGAMBO WA GAZA WAZIRI MKUU WA ISRAEL BENJAMINI NETANYAHU AWAONYA WANAMGAMBO WA GAZA Reviewed by safina radio on November 13, 2017 Rating: 5

No comments