MAMIA YA WAHAMIAJI WAOKOLEWA KATIKA PWANI YA LIBYA
TAREHE 1-11-2017
Mamia ya wahamiaji wameokolewa katika pwani ya
Libya,ambapo Maafisa wa polisi nchini humo wamesema kuwa jumla ya wahamiaji 300
wengi wao wakiwa ni kutoka mataifa ya kusini mwa Jangwa la Sahara, wameokolewa
jana katika boti mbili na kupelekwa kwenye ufukwe kwa Tripoli ambako walipatiwa
matibabu na msaada.
Mlinzi mmoja wa pwani amesema kuwa jumla ya watoto 15 na wanawake 25 ni miongoni mwa
wahamiaji waliookolewa.
Shirika la Umoja wa
Mataifa la Wahamiaji, IOM linakadiria kuwa zaidi ya wahamiaji laki moja wengi wao wakiwa kutoka Libya, wamevuka bahari
na kwenda Italia kwa mwaka huu, huku kiasi ya wahamiaji elfu kumi na nane
wakiwa wamezuiwa.
MAMIA YA WAHAMIAJI WAOKOLEWA KATIKA PWANI YA LIBYA
Reviewed by safina radio
on
November 01, 2017
Rating:

No comments