WAZIRI MKUU WA TANZANIA MH. MAJALIWA KASSIM MAJALIWA AELEZA SABABU ZA UPUNGUFU WA WATUMISHI KATIKA SEKTA MBALIMBALI.
TAREHE 16-11-2017
Waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh
Majaliwa Kassimu Majaliwa amesema kuwa upungufu wa watumishi katika sekta
mbalimbali za umma umetokana na zoezi la serikali la kuwaondoa watumishi hewa
pamoja na wenye vyeti vya kugushi.
Mh Majaliwa ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma
wakati akijibu maswali ya wabunge waliotaka kujua ni serikali itawaajiri watendaji wa vijiji na kata hapa nchini ili fedha
za miradi zinazopelekwa katika maeneo yao ziweze kusimamiwa vizuri na kutumika
kama ilivyopangwa.
Amesema kuwa zoezi la kuwaondoa watumishi hao
lilisababisha kutokea kwa upungufu wa rasilimali watu katika sekta mbalimbali
ikiwemo afya na elimu lakini kwa sasa serikali imetangaza kuwaajiri watumishi
wengine wapya zaidi ya elfu hamsini na mbili watakaojaza nafasi hizo.
Kuhusu upungufu wa watendaji wa mitaa na kata Mh
waziri mkuu amesema kuwa kazi ya kuaajiri watendaji hao hufanywa na halmashauri
za wilaya kutokana na uhitaji wao na bajeti waliojiwekea ili fedha zinazopaswa
kusimamiwa na viongozi hao wa kata na vijiji ziweze kusimaiwa vizuri.
Hata hivyo amesema kuwa azma ya serikali ya awamu ya
tano ni kuhakikisha kila sekta hapa nchini inapata watumishi wa kutosha na kwa
sasa rais ameshaanza kutoa kibali ajira katika sekta za afya,elimu na jeshi.
WAZIRI MKUU WA TANZANIA MH. MAJALIWA KASSIM MAJALIWA AELEZA SABABU ZA UPUNGUFU WA WATUMISHI KATIKA SEKTA MBALIMBALI.
Reviewed by safina radio
on
November 16, 2017
Rating:

No comments