ZAIDI YA SHILINGI BILIONI BILIONI ZATOLEWA KWA UJENZI WA MAEGESHO YA KIVUKO CHA LINDI-KITUNDA.
LINDI.
Serikali imetoa zaidi shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa
mradi wa maegesho ya Kivuko cha Lindi-Kitunda ili kuwawezesha wananchi wa Kitunda
kutekeleza shughuli zao za kiuchumi kwa ufanisi mkubwa.
![]() |
Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa Mnyaa. |
Hayo yameelezwa na Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na
Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa Mnyaa wakati akikagua ujenzi wa mradi huo katika
ziara yake ya siku moja mkoani Lindi.
Amesema kuwa wanachi wa eneo hilo walikuwa
wanachangamoto nyingi hasa kipindi bahari ikichafuka ambapo walikuwa wakipata
ugumu katika kusafiri kutoka upande mmoja kwenda mwingine.
Pia, ameongeza kuwa upatikanaji wa huduma za msingi
za kijamii kwa wananchi ulikuwa ukipatikana kwa ugumu hasa huduma za afya
kutokana na kutokuwapo kwa mawasiliano rafiki ya usafiri ya moja kwa moja
kutoka Kitunda kwenda Lindi kwa kuwa hudumu nyingi zinapatikana Lindi.
Hali kadhalika, amesema kuwa serikali ya awamu ya
tano imelitambua suala hilo na iliahidi kujenga maegesho ya kivuko pamoja na
kuleta kivuko ambapo ujenzi wa kivuko umekamilika kwa asilimia tisini na tisa na
itakamilika mwishoni mwa wiki hii ili kukabidhiwa na Mkandarasi wa mradi huo.
Hata hivyo, baada ya kukamilika kwa maegesho hayo
hatua itakayofuata ni kuletwa kwa kivuko hicho kitakachotumika kuimarisha
mawasiliano kati ya Kitunda na Lindi.
ZAIDI YA SHILINGI BILIONI BILIONI ZATOLEWA KWA UJENZI WA MAEGESHO YA KIVUKO CHA LINDI-KITUNDA.
Reviewed by safina radio
on
March 06, 2018
Rating:

No comments