WAKURUGENZI WA TAASISI NA MASHIRIKA NCHINI WAASWA KUZINGATIA SHERIA, KANUNI, NA TARATIBU.
MWANZA.
Wakurugenzi wa Taasisi na Mashirika mbali mbali nchini
wanaohudhuria mafunzo ya utawala bora, wameaswa kuzingati sheria, kanuni na
taratibu katika utekelezaji wa majukumu yao ili mashirika na Taasisi wanazoziongoza
ziweze kufanikiwa.
![]() |
Mkurug
|
Kauli hiyo imetoleawa na Mkurug enzi Mtendaji wa Taasisi
ya Wakurugenzi Tanzania Said Kambi jijini Mwanza ambapo amewataka Wakurugenzi
hao kuzingatia mafunzo hayo ili kuboresha ufanisi unaozingatia utawala bora.
Aidha, amebainisha kuwa Wakurugenzi hao wanauwezo wa
kufanya kazi lakini jambo la msingi linalofanywa na Taasisi ya Wakurugenzi
Tanzania ni kuyaweka mafunzo katika sayansi ya mfumo na mpangilio.
Amefafanua kuwa mafanikio ya utawala bora yanategemea
mambo mawili katika utendaji wa bodi ambayo ni uwezo au ustadi na umahiri
pamoja na taratibu, kanuni na mifumo.
Hata hivyo, Mafunzo hayo ya siku tano yatagawanyika katika
makundi mawili ya mafunzo ya cheti kwa wakurugenzi hamsini na nane na mafunzo kwa
makatibu kumi na tano wa bodi ambao ni wanasheria.
WAKURUGENZI WA TAASISI NA MASHIRIKA NCHINI WAASWA KUZINGATIA SHERIA, KANUNI, NA TARATIBU.
Reviewed by safina radio
on
March 06, 2018
Rating:

No comments