RAIS MAGUFULI LEO AMEFUNGUA MKUTANO WA 11 WA BARAZA LA WAFANYABIASHARA.
Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh John
Magufuli leo amefungua mkutano wa 11 wa baraza la wafanyabiashara ikulu jijini
Dar-es-Salaam.
RAIS MAGUFULI |
Akifungua mkutano huo rais Magufuli amewataka
wafanyabiashara hao kujadili kwa uwazi changamoto wanazopitia ili serikali
iweze kuwasaidia na kukuza uchumi wa nchi.
Amesema kuwa serikali iko tayari kusikiliza
changamoto zinazowakabili wafanyabiashara ndio maana imeamua kukutana nao
wakiwa na mawaziri wa wizara zote pamoja na makatibu wakuu ambao watachukua changamoto hizo kwa ajili ya kuzifanyia kazi.
Kwa upande wake mwenyekiti wa baraza la
wafanyabiashara hapa nchini Dr Reginald Mengi amemshukuru rais Magufuli kwa juhudi
zake za kupambana na rushwa juhudi ambazo zimesaidia kuleta ushindani wa kweli
katika sekta binafsi.
RAIS MAGUFULI LEO AMEFUNGUA MKUTANO WA 11 WA BARAZA LA WAFANYABIASHARA.
Reviewed by safina radio
on
March 19, 2018
Rating:
No comments