VIKUNDI VYA WANAWAKE NA VIJANA WILAYANI TARIME KUCHUKULIWA HATUA.
Mkuu wa wilaya ya Tarime Mkoani Mara Bw Glorias Luoga amesema kuwa
serikali itavichukulia hatua za kisheria ikiwemo kufikishwa mahakamani vikundi
vya wanawake na vijana ambavyo vilichukua mkopo na kushindwa kurejesha kwa
wakati.
Mkuu wa wilaya ya Tarime Mkoani Mara Bw Glorias Luoga |
Bw Luoga ametoa kauli hivyo wilayani humo wakati akikabidhi hundi ya
shilingi milioni ishirini na moja kwa vikundi 11 vya akina mama na vijana wa
halmashauri ya mji wa Tarime.
Amesema kuwa fedha walizokopeshwa wanawake na vijana hao ni asilimia kumi
ya mapato ya ndani ya halmashauri ya mji wa Tarime yaliyokusanywa kutoka kwenye
vyanzo vyake vya ndani.
Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri hiyo Bw Hamis Nyaswi amesmema
kuwa serikali imedhamiria kuwawezesha
wananchi kuwa na shughuli za kuwainua kiuchumi hivyo haina mzaha na fedha hizo.
VIKUNDI VYA WANAWAKE NA VIJANA WILAYANI TARIME KUCHUKULIWA HATUA.
Reviewed by safina radio
on
March 20, 2018
Rating:
No comments