CANADA KUTOA NDEGE ZA KIVITA NCHINI MALI


Nchi ya Canada imesema itatuma ndege kadhaa za kivita na zile za kusafirisha mizigo pamoja na wanajeshi watakaotoa mafunzo nchini Mali katika kipindi cha miezi 12 kusaidia operesheni inayoendelea kufanywa na walinda amani wa umoja wa Mataifa.

Image result for PICHA YA HELIKOPTA ZA KIVITA
Waziri wa ulinzi wa Canada, Harjit Sajjan amewaambia waandishi wa habari kuwa kikosi hicho maalumu kitajumuisha Helkopta mbili kubwa za kivita ambazo zinahitajika kwa sasa kwaajili ya usafirishaji pamoja na helkopta nyingine nne za kuendesha mashambulizi na kulinda misafara ya walinda amani.
Hata hivyo tarehe rasmi ya operesheni hii ya kwanza ya Canada barani Afrika tangu misheni yake ya nchini Rwanda na Somalia katika miaka ya 1990 pamoja na idadi kamili ya wanajeshi watakaotumwa, haijawekwa wazi.
Hakikisho hili la Canada limekuja baada ya mwaka uliopita Serikali ya Ottawa kusema kuwa ingetuma ndege za kivita na zile za usafirishaji kusaidia operesheni za ukanda mjini Entebbe Uganda pamoja na kuweka tayari kikosi chake kitakachosaidia operesheni za umoja wa Mataifa kilichokuwa na wanajeshi 200.
Waziri wa mambo ya nje wa Canada Chrystia Freeland amesema kuwa kikosi kitakachotumwa nchini Mali kitajumuisha wanawake ili kufikia lengo la usawa wa kijinsia kwenye operesheni za umoja wa Mataifa za kulinda amani.

CANADA KUTOA NDEGE ZA KIVITA NCHINI MALI CANADA KUTOA NDEGE ZA KIVITA NCHINI MALI Reviewed by safina radio on March 20, 2018 Rating: 5

No comments