IMEBAINISHWA KUWA NGUVU YA ROHO YA UDHAIFU HUWASHAMBULIA WATU WENYE MSAADA KWENYE FAMILIA.


Imebainishwa kuwa nguvu ya roho ya udhaifu huwashambulia watu wanaotegemewa kwenye familia ili kuharibu uchumi na mwelekeo wa maisha yao kwa njia ya magonjwa, zinaa, ulevi, madeni, hasira na migogoro.

Huduma ya redio Safina Kesho katika ukumbi wa Maombi uliopo Mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita mchana imekuandalia maombi ya  maalumu ya kuharibu msingi wa roho ya udhaifu uliojengwa ndani ya watu.


Aidha, udhaifu wa kiroho huja ndani ya mtu iwapo mtu hana neno la Mungu la kutosha, Nguvu za Mungu, Imani timilifu juu ya neno, Yesu Kristo ndani yake ikiwa ni pamoja na damu ya Yesu na tabia ya maombi.

Vile vile, nguvu ya roho ya udhaifu imeonekana kuwatesa watu kwa magonjwa, madeni, ndoa kuvunjika, biashara, pamoja na kuyumba kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja hadi familia.

Hata hivyo kesho watu wataombewa kulingana na mahitaji yao hivyo kila mmoja anashauriwa kuwa na imani pamoja na kujipatanisha na Mungu kwa njia ya maombi ya toba ili Mungu awaze kuwaokoa dhidi ya matatizo hayo yanayowakabili.

IMEBAINISHWA KUWA NGUVU YA ROHO YA UDHAIFU HUWASHAMBULIA WATU WENYE MSAADA KWENYE FAMILIA. IMEBAINISHWA KUWA NGUVU YA ROHO YA UDHAIFU HUWASHAMBULIA WATU WENYE MSAADA KWENYE FAMILIA. Reviewed by safina radio on March 26, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.