WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI WATAKIWA KUEPUKANA NA IMANI ZA KISHIRIKINA..
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Bi Zainabu Talak amezitaka
shule zote za msingi na sekondari mkoani humo kuwafundisha wanafunzi wao somo
la dini katika shule zao ili wawe na hofu ya Mungu na kuepukana na imani potofu
za kishirikiana.
Wanafunzi wakijifunza. |
Bi Talak ametoa maagizo hayo wakati wa ziara yake ya
kikazi wilayani Kishapu mkoani humo ambapo alitembelea miradi mbalimbali ya
maendeleo ikiwemo ya afya na ya maji.
Amesema kuwa wananchi wengi wamekuwa hawahudhurii
katika vituo vya afya vya matibabu kwa sababu ya kuamini imani potofu hivyo
kuanzia sasa shule zote za msingi na sekondari ni lazima pawepo na somo la dini
ili wanafunzi hao wawe na hofu ya Mungu.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya hiyo Nyamaganga
Taraba amewataka wananchi wa wilaya hiyo kuhudhuria katika vituo vya afya pindi
wanapokumbwa na magonjwa badala ya kwenda kwa waganga wa kienyeji kwani nyakati
hizi ni za sayansi na tekinolojia.
WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI WATAKIWA KUEPUKANA NA IMANI ZA KISHIRIKINA..
Reviewed by safina radio
on
March 16, 2018
Rating:
No comments