GAMBO APATA WASAA WA KUSIKILIZA CHANGAMOTO MBALI MBALI ZINAZOKABILI VIWANDA, ARUSHA.
Mkuu wa
mkoa wa Arusha Bw. Mrisho Gambo ameanza ziara ya siku tatu
ya kutembelea baadhi ya viwanda vipya na kujionea changamoto zinazo
kabili viwanda hivyo ambavyo vinatarajiwa kuaza kazi ya
uzalishaji wa bidhaa mbalimbali na kufikia malengo ya serikali ya kuwa na
uchumi wa kati.
Akizungumza
kwenye moja ya kiwanda kipya cha kuzalisha spea za pikipiki kilichopo eneo la Themi
halmashauri ya jiji la Arusha, Bw. Gambo alipata furusa ya kusikiliza
changamoto mbalimbali zinazokabili kiwanda hicho na kuzitolea ufafanuzi.
Katika
ziara hiyo pia Bw. Gambo ametembelea kiwanda cha kuzalisha mifuko cha kampuni
ya Mornaban ambapo mkurugenzi wa fedha wa kampuni hiyo Nathan Mollel
amesema kuwa kiwanda hicho kitagharimu zaidi ya shilingi bilioni tisa hadi kukamilika
kwake pamoja na changamoto zinazowakabilia.
Hata
hivyo, ziara hiyo ya mkuu wa mkoa wa Arusha ya ukaguzi wa
viwanda vipya, imekuja baada ya Rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli ya kuwataka wakuu wa mikoa yote nchini
kuhakikisha kila mkoa unakuwa na viwanda 100 mpaka ifikapo mwisho wa mwaka huu.
GAMBO APATA WASAA WA KUSIKILIZA CHANGAMOTO MBALI MBALI ZINAZOKABILI VIWANDA, ARUSHA.
Reviewed by safina radio
on
March 22, 2018
Rating:
No comments