IGP SAIMON SIRRO AWATAKA WAKANDARASI WANAOJENGA MIRADI YA JESHI HILO MKOANI DODOMA KUMALIZA KWA WAKATI.


Mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Saimon Sirro amewataka wakandarasi wanaojenga miradi ya jeshi hilo mkoani Dodoma kumaliza kazi hiyo kwa wakati ili kuwezasha azma ya serikali kuhamia Dodoma.



Image result for PICHA YA IGP SIMON SIRRO
IGP Saimon Sirro

IGP Sirro ameyasema hayo mkoani Dodoma wakati akikagua baadhi ya miradi ikiwemo nyumba thelathini za askari pamoja na jengo la makazi yake kwa kupitia mradi wa unaotekelezwa kwa kutumia wataalamu wa jeshi hilo.

Aidha, amebainisha kuwa katika ujenzi wa mradi huo unaoendela kujengwa na wataalaumu wa ndani wa jeshi hilo hadi sasa wametumia robo ya fedha za zilizotengwa huku akiwapongeza wakandarasi hao.

Amesema kuwa jambo la msingi ni wakandarasi hao ni kuendana na muda ili kufanikisha mradi huo kwa haraka kwa ajili ya kuimarisha usalama mkoani Dodoma kutokana na ongezeko la Watu katika Makao makuu ya nchi.

Hata hivyo, amewataka vijana waliopata ajira katika mradi huo kuwa wazalendo pamoja na kutokujihusisha na vitendo vya kihalifu katika kulinda vifaa vya ujenzi.

IGP SAIMON SIRRO AWATAKA WAKANDARASI WANAOJENGA MIRADI YA JESHI HILO MKOANI DODOMA KUMALIZA KWA WAKATI. IGP SAIMON SIRRO AWATAKA WAKANDARASI WANAOJENGA MIRADI YA JESHI HILO MKOANI DODOMA KUMALIZA KWA WAKATI. Reviewed by safina radio on March 16, 2018 Rating: 5

No comments