SERIKALI ZANZIBAR ITAENDELEA KUWASAIDIA WAWEKEZAJI WA NDANI.


Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema kuwa itaendelea kuwasaidia wawekezaji wa ndani ili waweze kuzalisha zaidi na kwenda sambamba na malengo ya serikali kufikia uchumi wa kati kupitia uchumi wa viwanda.

Image result for VIWANDA
Kwanda.
Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda Zanzibar Hassan Hamis baada ya Kamati ya  Biashara, Fedha na Kilimo kutembelea baadhi ya viwanda ikiwemo cha mifuko ya makaratasi na mjasiriamali wa kiwanda cha kufuga ng’ombe cha Mchui ambapo amesema kuwa serikali imejidhatiti kufufua viwanda ili kukuza uchumi wa nchi.

Mh Hamis amewataka wawekezaji wanaotaka kuanzisha viwanda hivyo waweze kushirikiana na serikali ili kukamilisha uwekezaji huo kwa ajili ya kuhakikisha kuwa azma na lengo la serikali ya Zanzibar ya Viwanda inatekelezeka kwa kasi inayohitajika.

Hata hivyo baadhi ya viongozi wa kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi ikiongozwa na Kaimu Mwenyekiti Hamad Abdala Rashidi wameishauri serikali kuweka tozo kubwa kwa biashara zinazotoka nje.

SERIKALI ZANZIBAR ITAENDELEA KUWASAIDIA WAWEKEZAJI WA NDANI. SERIKALI ZANZIBAR ITAENDELEA KUWASAIDIA WAWEKEZAJI WA NDANI. Reviewed by safina radio on March 26, 2018 Rating: 5

No comments