DOKTA AHMED ATEULIWA KUCHUKUA NAFASI DESALEGN NCHINI ETHIOPIA.


Mkutano wa  wa viongozi wa muungano tawala wa Ethiopian People's Revolutionary Democratic Front (EPRDF), umemteua Dokta Abiy Ahmed kuwa mwenyekiti wa Muungano huo.
Dkt. Abiy Ahmed
DOKTA AHMED
Dokta  Ahmed, anayetoka jamii ya Oromo yenye watu wengi Ethiopia, amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa muungano unaotawala EPRDF, hatua itakayomfanya kuwa Waziri Mkuu mpya wa nchi hiyo.
Ahmed alichaguliwa kwa zaidi ya asilimia 60 ya kura zilizopigwa kwa mujibu wa vyombo vya habari vya serikali na atachukua wadhifa huo kutoka kwa Hailemariam Desalegn aliyetangaza ghafla kujiuzulu mwezi uliopita.
Taifa hilo kwa sasa liko katika hali ya dharura iliyotangazwa kwa ajili ya kumaliza maandamano ya takriban miaka mitatu dhidi ya serikali.
Hata hivyo wakosoaji wake  wanasema ni mtu wa ndani katika chama na hivyo  hakuna matumaini kwamba matakwa ambayo yamekuwa yakiitishwa na waandamanaji kuwa yatatekelezwa.

DOKTA AHMED ATEULIWA KUCHUKUA NAFASI DESALEGN NCHINI ETHIOPIA. DOKTA AHMED ATEULIWA KUCHUKUA NAFASI DESALEGN NCHINI ETHIOPIA. Reviewed by safina radio on March 28, 2018 Rating: 5

No comments