TRA YAANZISHA MFUMO WA PAMOJA.


Mamlaka ya Mapato Nchini TRA imeanzisha mfumo wa pamoja unaolenga kuondoa changamoto zilizopo katika sekta ya biashara zikiwemo ucheleweshaji wa bidhaa bandarini.

Image result for PICHA YA KAMISHNA MKUU WA TRA CHARLES KICHERE
KAMISHINA MKUU TRA CHARLES KICHERE

Hayo yamebainika katika kongamano lililokutanisha wakuu wa taasisi za serikali na sekta binafsi utakao lenga kuondoa vikwazo katika taasisi hizo na kuboresha mazingira ya kibiashara.

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Nchini TRA Bw Charles Kichere amesema kuwa mradi wa mfumo wa pamoja utaongeza na kurahisisha utozaji wa tozo na katika sekta binafsi utapunguza gharama za upakuaji wa bidhaa forodhani.

Hata hivyo Mradi huo unatajwa kuwa hatua muhimu kwa serikali kushirikiana na taasisi mbali mbali pamoja na kuleta ufanisi kwa watu wanaopelekewa huduma ambapo mfumo huo utalenga maeneo muhimu ikiwemo usimamizi wa mapato, utekelezaji wa sera za biashara, usalama wa uwekezaji na ugawaji wa bidhaa pamoja na uchukuzi bandarini na viwanja vya ndege.

TRA YAANZISHA MFUMO WA PAMOJA. TRA YAANZISHA MFUMO WA PAMOJA. Reviewed by safina radio on March 29, 2018 Rating: 5

No comments