MZOZO WA SYRIA WAINGIA MWAKA WA NANE.
Mzozo wa Syria umeingia mwaka wa
nane leo huku Uturuki ikilizingira eneo la Wakurdi upande wa Kaskazini hhuku vikosi
vya serikali vikiyashambulia maeneo ya waasi karibu na mji mkuu Damascus.
Katika mapigano ya hivi karibuni vikosi
vinavyoungwa mkono na Uturuki vimefanya mashambulio ya mabomu katika mji wa
Afrin na kukaribia kuuzingira mji huo, katika uvamizi ambao huenda ukaibadili
ramani ya kaskazini mwa Syria.
Jeshi Syria leo limethibitisha kuingia katika
eneo la Ghouta Mashariki ambapo Urusi imesema imerefusha usitishaji mapigano
kwa siku mbili katika mji wa Douma kwenye eneo hilo ili kuruhusu misaada ya
kibinadamu.
Hata hivyo mjumbe maalumu wa Umoja
wa Mataifa kwa ajili ya mzozo wa Syria Staffan de Mistura anatarajiwa
kulihutubia baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu mzozo huo.
MZOZO WA SYRIA WAINGIA MWAKA WA NANE.
Reviewed by safina radio
on
March 15, 2018
Rating:
No comments