RAIS MAGUFULI AMEWATAKA WATENDAJI WA SERIKALI KUSHIRIKIANA NA WAWEKEZAJI.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli
amewataka watendaji wa serikali wakiwemo mawaziri na wakuu wa mikoa kuhakikisha
wanashirikiana na wawekezaji ili kuimarisha uchumi kupitia viwanda vya ndani.
RAIS MAGUFULI. |
Mh Magufuli ametoa maagizo hayo leo mkoani Morogoro
wakati akizindua kiwanda cha Philips Moris International kinacho endeshwa na
Kampuni ya Mansur Industries mkoani humo na kuwataka watanzania kuthamini
bidhaa za ndani ili kukuza uchumi wa nchi.
Aidha, Rais Magufuli amewataka watanzania kubadili
dhana ya kufikiria kuwa Tanzania ni soko la kuuza malighafi za nje ya nchi bali
mtazamo wao uwe katika kujenga viwanda ndani ya nchi ili kufanya mabadiliko ya
mapinduzi ya kiuchumi.
Hata hivyo, ameahidi kushughulikia uwepo wa kero za kodi na ushuru mwingi unaotozwa
kwa bidhaa zinazozalishwa na viwandwa vya ndani pamoja na uingizwaji wa bidhaa
nyingi kutoka nje ya nchi ili kulinda uwekezaji kupitia viwanda vya ndani
sambamba na kuimarisha ushindani wa soko la ndani.
Kwa upande wake waziri wa viwanda na uwekezaji nchini
Mh Charles Mwijage amemuomba rais Magufuli kutembelea viwanda
vilivyokamilika,huku mkuu wa mkoa wa Morogoro Dr Kebwe Stephen Kebwe akisema
kuwa mkoa huo umepiga hatua katika uchumi wa viwanda.
RAIS MAGUFULI AMEWATAKA WATENDAJI WA SERIKALI KUSHIRIKIANA NA WAWEKEZAJI.
Reviewed by safina radio
on
March 15, 2018
Rating:
No comments