JESHI LA POLISI LIMESEMA LIMEJIPANGA KIKAMILIFU KKUIMARISHA ULINZI KATIKA KIPINDI HIKI CHA PASAKA



Jeshi la Polisi Nchini limewahakikishia wananchi kuwa limejipanga kikamilifu kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama katika kuimarisha ulinzi na usalama katika kipindi cha siku kuu ya pasaka.

Image result for PICHA YA IGP SIRRO
IGP SIRRO
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari Inspekta Jenerali wa polisi IGP Saimon Sirro amesema kuwa askari wa jeshi hilo wamejipanga vizuri ili kudhibiti vitendo vya kihalifu visifanyike na vitakapojitokeza vitadhibitiwa kwa haraka.

Aidha, Kamanda Sirro amewataka wamiliki wa kumbi za starehe kufuata sheria kanuni na taratibu za uendeshaji wa kumbi hizo ikiwemo kutoruhusu Disko Toto, na kujaza watu kupita kiasi huku wazazi wakitakiwa kuwaangalia watoto wao na kutokuwaacha wenyewe bila uangalizi.

JESHI LA POLISI LIMESEMA LIMEJIPANGA KIKAMILIFU KKUIMARISHA ULINZI KATIKA KIPINDI HIKI CHA PASAKA JESHI LA POLISI LIMESEMA LIMEJIPANGA KIKAMILIFU KKUIMARISHA ULINZI KATIKA KIPINDI HIKI CHA PASAKA Reviewed by safina radio on March 28, 2018 Rating: 5

No comments