SERIKALI DRC YAKATAA MSAADA WA EU KUTOKANA NA UMOJA HUO KUONGEZA CHUMVI KATIKA MASUALA YA KIBINADAMU.


Umoja wa Ulaya umesema unaguswa na nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya nchi hiyo kutangaza kuwa itakataa kupokea kiasi cha dola za Marekani bilioni 1 na laki 7 ambazo ni msaada wa kimataifa.
Image result for Umoja wa Ulaya
Bendera za Umoja wa Ulaya zikipepea katika Ofisi za Makao Makuu ya huo mjini Brussels.
Mvutano wa maneno umeibuka kati ya umoja wa Mataifa na Serikali ya DRC baada ya utawala wa Kinshasa Ijumaa ya wiki iliyopita kusema haitashiriki mkutano wa kimataifa wa kuisaidia nchi hiyo fedha za misaada ya kibinadamu mjini Geneva, Uswis, Serikali ikisema tatizo la kibinadamu limeongezwa chumvi kuliko hali halisi.
Umoja wa Ulaya unaguswa na kuzorota kwa hali ya kibinadamu nchini DRC, amesema mkuu wa masuala ya kibinadamu kutoka umoja wa Ulaya Christos Stylianides wakati akizungumza na wanahabari kwenye mji wa Goma.
Waziri mkuu wa DRC Jose Makila alinukuliwa siku ya Ijumaa ya wiki iliyopita akisema umoja wa Mataifa umoengeza chumvi na kwamba mashirika yake ya misaada na asasi za kiraia zimekuwa zikifanya propaganda ya kuichafua nchi yake.



SERIKALI DRC YAKATAA MSAADA WA EU KUTOKANA NA UMOJA HUO KUONGEZA CHUMVI KATIKA MASUALA YA KIBINADAMU. SERIKALI DRC YAKATAA MSAADA WA EU KUTOKANA NA UMOJA HUO KUONGEZA CHUMVI KATIKA MASUALA YA KIBINADAMU. Reviewed by safina radio on March 26, 2018 Rating: 5

No comments