RAIS MAGUFULI AMWAGIZA WAZIRI WA TAMISEMI KUWASIMAMISHA KAZI WAKURUGENZI WAWILI


Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh John Magufuli amemwagiza waziri wa nchi ofisi ya rais TAMISEMI Mh Suleman Jaffo kuwasimamisha kazi wakurugenzi wa halmashauri za wilaya ya Ujiji mkoani Kigoma na Pangani mkoani Tanga kufuatia matumizi mabaya ya fedha za serikali.

Image result for PICHA YA RAIS MAGUFULI
RAIS MAGUFULI.

Mh Magufuli ametoa maagizo hayo leo ikulu jijini Dar-es-salaam baada ya kupokea ripoti ya fedha ya mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG Professa Juma Mussa Hassad,ambapo amesema kuwa serikali itaendelea kuwachukulia hatua zaidi viongozi wanaoshindwa kusimamia matumizi mazuri ya fedha za umma.

Amesema kuwa katika ripoti hiyo ya CAG Halmashauri hizo zilipata hati chafu hivyo ni lazima wakurugenzi hao wakae pembeni ili kupisha uchunguzi huku akimtaka waziri mkuu Mh Kassimu Majaliwa kushirikiana na mawaziri kupitia ripoti hiyo ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.

Kwa upande wake waziri mkuu Mh Kasimu Majaliwa ameahidi kuifanyia kazi ripoti hiyo ili mapungufu yaliyojitokeza yasijitokeze tena wakati mwingine.

Akisoma ripoti hiyo mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG Professa Juma Mussa Hassad amesema kuwa katika ukaguzi wao wamebaini kuwa mashirika ya umma na serikali za mitaa zimefanya vizuri tofauti na hapo awali hali inayoonyesha kuwa fedha za umma zinatumika vizuri.

RAIS MAGUFULI AMWAGIZA WAZIRI WA TAMISEMI KUWASIMAMISHA KAZI WAKURUGENZI WAWILI RAIS MAGUFULI AMWAGIZA WAZIRI WA TAMISEMI KUWASIMAMISHA KAZI WAKURUGENZI WAWILI Reviewed by safina radio on March 27, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.