KINARA WA UPINZANI NCHINI SIERRA LEONE AMTUHUMU RAIS ANAYEMALIZA MUDA WAKE.


Kinara wa upinzani nchini Sierra Leone Julius Maada Bio amemtuhumu rais anayemaliza muda wake Ernest Bai Koroma kwa kujaribu kuchelewesha kwa makusudi uchaguzi wa duru ya pili uliopangwa kufanyika Jumanne ya wiki hii kwa kwenda mahakamani kujaribu kukifanya chama tawala kibaki madarakani.

Image result for PICHA YA JULIUS MAADA BIO KINARA WA UPINZANI NCHINI SIERRA LEONE
KINARA WA UPINZA MAADA BIO 
Mahakama kuu ya nchi hiyo mwishoni mwa juma iliiagiza tume ya taifa ya uchaguzi kusitisha maandalizi ya kura hiyo hadi pale kesi ya malalamiko ya uchaguzi itakaposikilizwa, kesi ambayo iliwasilishwa na mawakili wenye uhusiano na chama tawala.
Bio ambaye alishinda duru ya kwanza katika uchaguzi wa Machi 7 kupitia chama cha Sierra Leone People's, atashindana na Samura Kamara ambaye ni mgombea anayeungwa mkono na rais Koroma na anawakilisha chama tawala cha All People's Congress.
Bio amesema Koroma atalazimika kuwajibika kwa chochote kitakachotokea baadae, kuchelewa au kufutwa kwa uchaguzi kunakotengeneza hofu ya kusababisha machafuko nchini humo.
Chama tawala cha APC kinategemea wapiga kura wa kaskazini mwa nchi hiyo kwenye miji Temne na Limba wakati chama cha upinzani cha SLPP chenyewe kina umaarufu mkubwa kusini mwa nchi hiyo hasa kwenye jamii ya Mende.

KINARA WA UPINZANI NCHINI SIERRA LEONE AMTUHUMU RAIS ANAYEMALIZA MUDA WAKE. KINARA WA UPINZANI NCHINI SIERRA LEONE AMTUHUMU RAIS ANAYEMALIZA MUDA WAKE. Reviewed by safina radio on March 26, 2018 Rating: 5

No comments