RAIS WA KOREA KASKAZINI AMEANZA ZIARA YAKE NCHINI CHINA


Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un ameanza ziara yake ya kwanza nje ya nchi tangu ashike madaraka mwaka 2011.
Image result for PICHA YA RAIS WA KOREA KASKAZINI
RAIS WA KOREA KASKAZINI KIM JONG UN
Ulinzi umeimarishwa mjini Beijing kama ambavyo hutokea  wakati viongozi wa China wanapokutana na viongozi wakuu wa mataifa ya kigeni.
Hatua hii inathibitisha taarifa za awali zilizotolewa na vyombo vya habari vya Japan kuwa afisa wa ngazi ya juu kutoka Korea Kaskazini amesafiri kwa treni kwenda China.
Hata hivyo msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China ameviambia vyombo vya habari kuwa hakuwa na taarifa iwapo Kim Jong Un anazuru nchini humo.
Ziara hiyo inakuja kabla ya Kim Jong Un kukutana na rais wa Korea Kusini Moon Jae-in mwezi ujao na ambayo huenda yakafuatiwa na mazungumzo kati ya kiongozi huyo wa Korea Kaskazini na rais wa Marekani Donald Trump yanayolenga kupunguza mivutano iliongezeka tangu Trump aingie madarakani.

RAIS WA KOREA KASKAZINI AMEANZA ZIARA YAKE NCHINI CHINA RAIS WA KOREA KASKAZINI AMEANZA ZIARA YAKE NCHINI CHINA Reviewed by safina radio on March 27, 2018 Rating: 5

No comments